Uploaded by Rev Mwakifwamba

ROHO MTAKATIFU BOOKLET

advertisement
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
Kitabu cha mafundisho ya ROHO MTAKATIFU ili kupokea nguvu ya
kukusaidia katika mafanikio ya kimwili na kiroho.
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
Kimeandikwa na:
Rev Anthony Mwakifwamba
+255 762 282 777 na +255 718 613 491
P.O. BOX 2256, Dodoma City, Tanzania
Na kuchapishwa na
Copyright ©2019
Haki zote zimehifadhiwa hauruhusiwi
kunakili, kunukulu wala kuchapisha maneno
ya kitabu hiki kwa lengo la kuuza kitabu hiki
bila idhini ya mwandishi.
1
sehemu ya kwanza
Roho Mtakatifu ni nani?
Kutokana na biblia katika agano la kale
a)
Roho Mtakatifu anatumbulishwa kama Roho ya Mungu
Mwanzo 1:1-2
Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Nayo nchi
ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi
vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
b)
Anatambulishwa kama uweza
Hesabu 11:26
Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa
Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi; na roho ile
ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandikwa,
lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri
kambini.
Kutoka 35:30-31
Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli, Angalieni, Bwana
amemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa
Huri, wa kabila ya Yuda; 31 naye amemjaza roho ya Mungu,
katika hekima, na akili, na ujuzi, na kazi ya ustadi kila aina;
c)
Roho mtakatifu anatambulishwa kama Muumbaji
Ayubu 33:4
Roho ya Mungu imeniumba, Na pumzi za Mwenyezi hunipa uhai.
Kutokana na biblia agano jipya.
2
a)
Anatangazwa rasmi kuwa ni mtenda kazi pamoja na
Mungu
Mathayo 3:11
Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye
ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata
kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu
na kwa moto.
Luka 3:16
Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa
maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi
sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa
Roho Mtakatifu na kwa moto;
Marko 1:8
Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho
Mtakatifu.
b)
Anatambulishwa kama kiongozi
Mathayo 4:1
Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.
Hii maana yake aliongozwa na Roho mpaka mlimani.
Luka 2:27
Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi
walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa
desturi ya sheria,
c)
Anajulikana kama msemaji ndani yetu
Mathayo 10:20
3
Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye
ndani yenu.
d)
Anajulikana kama mtoa pepo
Mathayo 12:28
Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa
Mungu umekwisha kuwajilia.
e)
Anajulikana kama Mwalimu
Luka 12:12
kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha saa ile ile yawapasayo
kuyasema.
f)
Anajukana kama ni Mungu lakini pia ni Yesu
Yohana 4:24
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu
katika roho na kweli.
2Korintho 3:17
Basi <Bwana> ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo
ndipo penye uhuru.
Warumi 8:26 na 34
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana
hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe
hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
34Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye
aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye
yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
Sasa hapa anajukana kama Yesu kwa sababu ya kutombea
kama tulivyotangulia pale kwenye Warumi 8:26.
4
g)
Anajulikana kama msaidizi
Yohana 14:26
Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba
atampeleka
kwa
jina
langu,
atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Rumi 8:26a
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu,
h)
Anajulikana kama Roho wa kweli
Yohana 16:13
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza
awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri
lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na
mambo yajayo atawapasha habari yake.
1Yohana 4:6
Sisi twatokana na Mungu. Yeye amjuaye Mungu atusikia; yeye
asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa
kweli, na roho ya upotevu
i)
Anajulikana kama nguvu itendayo kazi ndani yetu
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho
Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu,
na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
j)
Anajuliakana kama Roho wa Hekima
Matendo 6:10
lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho
aliyesema naye.
5
k)
Anajulikana kama mtoa vipawa
Matendo 2:38
Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina
lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea
kipawa cha Roho Mtakatifu.
1Korintho 12:8-9
Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na
mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; 9
mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za
kuponya katika Roho Yule mmoja;
l)
Anajulikana kama shuhuda ndani yetu
Warumi 8:16
Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi
tu watoto wa Mungu;
1Korintho 12:3
Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika
Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu
kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
Ebrania 10:15a
Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, …………
m)
Anajulikana kama mwombezi wetu
Warumi 8:26c
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana
hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe
hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
6
n)
Anajulikana kama Roho wa utakaso
Warumi 15:16
ili niwe mhudumu wa Kristo Yesu kati ya watu wa Mataifa,
niifanyie Injili ya Mungu kazi ya ukuhani, kusudi Mataifa wawe
sadaka yenye kibali, ikiisha kutakaswa na Roho Mtakatifu.
2Thesalonike 2:13
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili
yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu
amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa
na Roho, na kuiamini kweli;
o)
Anajulikana kama mchunguzi(mpelelezi)
1Korintho 2:10-11
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho
huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. 11 Maana ni nani
katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya
binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu
hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.
p)
Anajulikana kama mtenda kazi ndani yetu
1Korintho 12:11
lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule,
akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.
Roho Mtakatifu ni tofauti na malaika ambao wao
wanayomaumbo kamili japokuwa wakati mwingine
walijionyesha kama wanadamu wa kawaida, ila Roho Mtakatifu
yeye huja kama nguvu wala huwezi kumwona atakapokuja ila
utagundua kuwa amekuja kutokana na ile kazi atakayoifanya
ndani ya mtu au mahali pale Matendo 2:1-4 inasema Hata
7
ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. 2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa
nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa
wameketi. 3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama
ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. 4 Wote wakajazwa
Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama
Roho alivyowajalia kutamka.
Kazi za Roho Mtakatifu ni zipi?
Wakati anatambulishwa na Yesu kati ya wanafunzi wale
kumi na moja, Yesu anamtaja kama msaidizi atakayewasaidia
kufanya yote aliyowaamuru kuyafanya. Yohana 14:16-18
inasema Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi
mwingine, ili akae nanyi hata milele; 17 ndiye Roho wa kweli;
ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni
wala haumta-mbui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa
kwenu, naye atakuwa ndani yenu. 18 Sitawaacha ninyi yatima;
naja kwenu.
Kufundisha
Yohana 14:26
Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba
atampeleka
kwa
jina
langu,
atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Kutuongoza na kutupeleka kwenye kweli yote(kwenye
neo la Mungu)
8
Yohana 16:13
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza
awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri
lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na
mambo yajayo atawapasha habari yake.
Kutuombea
Warumi 8:26c
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana
hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe
hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Kutushuhudia ndani yetu
Warumi 8:16
Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi
tu watoto wa Mungu;
Kutuunganisha na mbingu
1Yohana 5:8-9
Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na
Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. 9 Kisha
wako watatu washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na
watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda
wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana
ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia
Mwanawe.
9
(Yupo mbinguni lakini yupo tena duniani).
Kuponya
1Korintho 12:9a
…………..na mwingine karama za kuponya katika Roho Yule
mmoja;
Kutupa nguvu ya kushindana na kila hali ya kipepo
Matendo 1:8a
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho
Mtakatifu;
Kutufunulia mafumbo ya mbingu na kutupasha habari ya
mambo yajayo
1Korintho 2:10
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho
huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.
Yohana 16:13
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza
awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri
lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na
mambo yajayo atawapasha habari yake.
10
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
sehemu ya pili
Roho Mtakatifu anakaa wapi?
Ukimwangalia katika nafasi ya Mungu utamwona yupo
mbinguni 1Yohana 5:8 inasema, Kwa maana wako watatu
washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na
watatu hawa ni umoja.
Lakini ukimtazama kama msaidizi utamwona yupo
duniani 1Yohana 5:9 inasema, 9 Kisha wako watatu
washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa
hupatana kwa habari moja.
Pia Roho Mtakatifu anaweza kuishi ndani ya mtu na
huyo mtu akajulikana kama hekalu 1Korintho 3:16; Hamjui
ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa
Mungu anakaa ndani yenu?
Na 1Korintho 6:19,20 inasema, Au hamjui ya kuwa
mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu,
mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20
maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu
katika miili yenu.
Kitendo cha Roho Mtakatifu kushuka na kukaa kwa mtu
kinajulikana kama kuvuviwa, ama uvuvio wa Roho Mtakatifu.
Yohana 20:22 inasema, Naye akiisha kusema hayo,
akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
Kwa kuwa Roho Mtakatifu haonekani katika umbo lake
basi anaposhuka anakuwa kama nguvu Fulani yenye utiisho
11
mkubwa, na akisha kaa ndani ya mtu, huyo mtu anajaa nguvu
au uwezo wa kufanya jambo Fulani, ndiyo maana tunasema
mtu huyu amejaa Roho Mtakatifu Matendo 2:4 inasema Wote
wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha
nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Na Mtendo 1:8. Inasema, Lakini mtapokea nguvu,
akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa
mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote,
na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Kwa mfano kama akitaka watu wajifunze neno la
Mungu basi anakuja kama mwalimu, ama akitaka kuponya
anakuja kama nguvu ya kuponya, akitaka kutoa unabii basi
utakuta anakuja kama nabii, na akishakuja ndani ya mtu lazima
huyo mtu awe kama mtu aliyetumwa na mamlaka isiyo ya
kwake.
Tunawezaje kumpokea Roho Mtakatifu?
Ili tuweze kujazwa na Roho Mtakatifu ni lazima tuwe
tumemwamini yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yetu
ndipo tufuate hatua zinazofuatia :
Kufundishwa Neno la Mungu ama kusikia Neno la Mungu.
Matendo 2:33-37
33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa
Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu,
amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia. 34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe
anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa
mkono wangu wa kuume. 35 Hata nitakapowaweka adui zako
12
chini ya miguu yako. 36 Basi nyumba yote ya Israeli na wajue
yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo
mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo. 37 Walipoyasikia haya
wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume
wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni
mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate
ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho
Mtakatifu.
Matendo 10:34,35,39-44
Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Hakika natambua ya
kuwa Mungu hana upendeleo; 35 bali katika kila taifa mtu
amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.
39 Nasi tu mashahidi wa mambo yote aliyoyatenda katika nchi
ya Wayahudi na katika Yerusalemu; ambaye walimwua
wakamtundika mtini. 40 Huyo Mungu alimfufua siku ya tatu,
akamjalia kudhihirika, 41 si kwa watu wote, bali kwa mashahidi
waliokuwa wamekwisha kuchaguliwa na Mungu, ndio sisi,
tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake
kutoka kwa wafu. 42 Akatuagiza tuwahubiri watu na
kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe
Mhukumu wa walio hai na wafu. 43 Huyo manabii wote
humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye
atapata ondoleo la dhambi. 44 Petro alipokuwa akisema
maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile
neno.
13
Kwa kuwekewa mikono
Matendo 8:14-16
Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba
Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na
Yohana; 15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee
Roho Mtakatifu; 16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja
wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.
Matendo 19:2-6
akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?
Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu
hatukusikia. 3 Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani?
Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana. 4 Paulo akasema, Yohana
alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini
yeye
atakayekuja
nyuma
yake,
yaani,
Yesu.
5 Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu. 6 Na
Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu
akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.
Kusoma Neno la Mungu na kuomba
Matendo 4:31
Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale
walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu,
wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
14
Kumtukuza, kumshukuru na kumsifu Yesu Kristo kwa
muda mrefu.
Yohana 7:39
Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale
wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa
hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
NB: Roho mtakatifu hatolewi kwa kipimo bali anatolewa kwa
imani, Yohana 3:34 inasema, Kwa kuwa yeye aliyetumwa na
Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho
kwa kipimo.
Pia unapompokea Roho Mtakatifu anakupa na karama
zake wala Roho Mtakatifu hatoi karama zake kwa fedha bali
kwa kutubia uovu au dhambi na kunyenyekea mbele zake
mkimtafuta yeye zaidi kuliko kuvitafuta vitu vyake, Matendo
8:18-22 inasema, Hata Simoni alipoona ya kuwa watu
wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya mitume,
akataka kuwapa fedha akisema, 19 Nipeni na mimi uwezo huu,
ili kila mtu nitakayemwekea mikono yangu, apokee Roho
Mtakatifu. 20 Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee
mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya
Mungu yapatikana kwa mali. 21 Huna fungu wala huna sehemu
katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za
Mungu.22 Basi, tubia uovu wako huu, ukamwombe Bwana, ili
kama yamkini, usamehewe fikira hii ya moyo wako.
15
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
sehemu ya Tatu
Dalili za mtu aliyempokea Roho Mtakatifu
Kwa kuwa Roho Mtakatifu hujidhihirisha kama nguvu,
basi kuna sababu zote kuwa anapokushukia utakuwa na dalili
za kushukiwa, tuzitazame hizi dalili:
a)
Kunena kwa Lugha ambayo kikawaida hujawahi
kusema hapo kwanza
Matendo 2:4
Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha
nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Matendo 10:44-46
Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu
akawashukia wote waliolisikia lile neno. 45 Na wale
waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja
pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa
kipawa cha Roho Mtakatifu.46 Kwa maana waliwasikia
wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu..................
b)
Unahisi nguvu ndani yako inayokupa ujasiri katika
mambo ya Kiroho yanayolingana na maagizo ya Yesu.
Matendo 4:31
16
Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale
walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu,
wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
c)
Unapata awezo wa kushinda mambo ya kale kabla
ya kumpokea Yesu, ulikuwa mlevi, mvuta sigara
nakadhalika, sasa unajikuta ukiwa kama mtu mpya,
ambapo tunaita kuzaliwa upya katika roho.
Yohana 3:5,8
Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee?
Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa? 5
Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji
na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. 6
Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni
roho. 8 Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini
hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila
mtu aliyezaliwa kwa Roho.
Matendo 1:5
ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa
katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.
d)
Unapata Uhuru mkubwa nafsini mwako, na uhuru
huu hauwezi kuvuka mipaka ya Neno la Mungu.
2Korintho 3:17
Basi <Bwana> ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo
ndipo penye uhuru.
17
Warumi 8:21
kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa
katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa
utukufu wa watoto wa Mungu.
Yohana 8:34-36
Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi
ni mtumwa wa dhambi. 35Wala mtumwa hakai nyumbani siku
zote; mwana hukaa siku zote. 36 Basi Mwana akiwaweka huru,
mtakuwa huru kweli kweli.
e)
Utii wa Neno la Mungu unaongezeka ndani yako, na
utii wa uongozi wa Roho Mtakatifu kwa watu wengine
waliojazwa na Roho Mtakatifu kama wewe unazidishwa.
1Korintho 14:32-33
Na roho za manabii huwatii manabii. Kwa maana Mungu si
Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo
katika makanisa yote ya watakatifu.
Dalili zinazoashiria kuwa unaroho zidanganyazo ambazo
zinajifanya kuwa ni Roho Mtakatifu.
a)
Huwezi kujazwa na Roho halafu ukamsema vibaya Yesu
Kristo, ama ukakosoa maandiko ya uzima na Neno la Mungu.
18
1Korintho 12:3
Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika
Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu
kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
b)
Mara baada ya kile unachohisi umejazwa na Roho
halafu ukawa kila ukiomba unahamishwa ufahamu wako
na kutokujielewa katika maombi, ujue hapo ni roho
zingine zilizo ndani yako(kutokujitambua wakati wa
maombi).
Maana baada ya kumpokea Roho Mtakatifu uombaji
wako unabadilishwa na kuomba kwa uhuru, wala fahamu zako
hazihamishwi, hivyo unakuwa unaomba kwa roho lakini pia
kwa akili.
1Korintho 14:15,33
Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili
pia; nitaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia. 33Kwa
maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile
kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.
c)
Mtu akiwa hajajazwa na Roho Mtakatifu hawezi
kunena kwa lugha, lakini pia kila atakapotoka kunena kwa
lugha au katika kuomba huwa hawezi kuwa na tunda la
Roho.
Bado anakuwa msengenyaji, chuki, hasira, mbinafsi na
matendo mengine yanayofanana na hayo au mwingine
anakuwa na hofu ndani yake, hawi huru, kwa sababu kile
kilichoko ndani yake ni roho zidanganyazo.
19
2Timotheo 1:7
Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya
upendo na ya moyo wa kiasi.
Warumi 8:15
Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali
mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba,
yaani, Baba.
d)
Hawezi kujizuia kutenda dhambi, ikiwa atatenda
dhambi nafsi yake inakuwa haina hukumu
Warumi 6:18
Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa
miili
yenu.
Kwa
kuwa
kama
mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate
kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki
mpate kutakaswa.
1Wakorintho 11:31-32
Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa. Ila
tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isije ikatupasa adhabu
pamoja na dunia.
e)
Mtu anafundishwa, na kukaa nyumbani mwa Bwana
lakini bado anaenenda gizani.
20
1Yohana 5:18
Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi;
bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu
hamgusi.
2Korintho 11:14
Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano
wa malaika wa nuru.
Matendo ya giza yanatajwa katika Waefeso 5:9-11 na
Wagalatia 5:16-21 kuwa ni: uasherati, uchafu, ufisadi, 20
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina,
faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana
na hayo, .
21
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
sehemu ya Nne
Usiziamini kila roho
Kuna roho zingine ni roho zidanganyazo wala si roho
zinazotokana na Mungu, hivyo tunapaswa kuzijaribu ikiwa
tunapatwa na mashaka nazo.
1Timotheo 4:1-3
Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho
wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo,
na mafundisho ya mashetani; 2 kwa unafiki wa watu wasemao
uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; 3 wakiwazuia
watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo
Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani
wenye kuijua hiyo kweli.
Hivyo hatupaswi kuziamini kila roho, tunaweza kuzitambua
kwa namna mbalimbali zikiwemo njia za kulinganisha
maandiko na hali za hizo roho.
1Yohana 4:3
Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo
roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa
imekwisha kuwako duniani.
Kwanza kabisa lazima kila roho inayotokana na Mungu
imkiri Kristo kuwa ni Mungu na alikufa na kufufuka, pia ndiye
atakayeuhukumu ulimwengu.
22
Yohana 8:31
Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi
mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli
kweli;
Kila nabii anapotoa unabii ujue ni Bwana anasema,
kama ni Bwana anasema basi ni lazima Neno la Bwana lihusike,
kama hakuna neno basi hakuna unabii; na kila nabii asiye
tumia maandiko ya neno la uzima ni mwongo.
Kumbukumbu la torati 18:20, 22
Lakini nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu,
ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la
miungu mingine, nabii yule atakufa.
22Atakaponena nabii kwa jina la Bwana, lisifuate jambo lile
wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena Bwana; kwa kujikinai
amelinena huyo nabii, usimwogope.
Nabii akinena jambo kwa kulitolea unabii na hilo jambo
lisitokee basi atakuwa amenena yeye mwenyewe kwa kujikinai
na wala Bwana hajasema, hivyo huyo nabii anaweza kuwa ni
nabii wa uongo ama asiyetaka kunena maneno kutoka kwa
Bwana, na neno usimwogope linaenda mbali zaidi ya kuogopa,
maana nyingine tunaweza kusema usimpokee.
Yohana 16:13
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza
awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri
lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na
mambo yajayo atawapasha habari yake.
23
Mtu atakayesema kama Mungu, yaani ikawa kama yeye
ndiye anayesema basi huyo ndiye nabii wa uongo, maana kila
nabii wa Mungu husema kama kinywa cha Mungu, anasema
kama mtu aliyetumwa kusema, hivyo kwake yeye kusema
Bwana kasema ni kawaida yake, na atakaposema huwa hatafuti
hekima nyingine zaidi ya ile aliyotumwa, na pia halazimishi
ujumbe wake upokelewe, maana kazi yake ni kusema tu wala si
kutaka atakayoyasema yafuatwe.
Mathayo 15:4
Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako,
na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
Mtu mwenye Roho Mtakatifu anafuata kanuni zote za
Yesu alizozisema, ikiwa mtu huyo atasema kwa lugha ya
malaika au lugha ya wanadamu na akawa hana heshima kwa
watu waliomzidi umri ama kuwadharau basi mtu huyo hana
Roho Mtakatifu badala yake anaroho zidanganyazo.
1Korintho 13:8
Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii
utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa,
yatabatilika.
Kanuni kuu kuliko zote ambazo Yesu alizitaka tuzifuate
ni upendo, kama mtu akiwa anafanya ishara za Roho Mtakatifu
halafu akawa hana upendo basi mtu huyo ni dhahili kabisa
kuwa hana Roho Mtakatifu bali anaroho zidanganyazo.
24
Wafilipi 2:3
Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali
kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora
kuliko nafsi yake.
Kutoka 35:29
Wana wa Israeli wakaleta sadaka za kumpa Bwana kwa moyo
wa kupenda; wote, waume kwa wake, ambao mioyo yao
iliwafanya kuwa wapenda kuleta kwa hiyo kazi, ambayo Bwana
aliamuru ifanywe kwa mkono wa Musa.
Roho Mtakatifu akishuka hutupeleka kwenye mapenzi
ya Mungu wala sisi hatujipeleki wenyewe, hivyo ndani yetu
tunaanza kupata shauku ya kutimiza yale anayoyataka wala si
kwa lazima ya mtu fulani, bali tunajikuta wenyewe tunavutwa
kufanya sawasawa na apendavyo Mungu.
Isaya 42:8
Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa
mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.
Galatia 5:25-26
Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. 26 Tusijisifu bure,
tukichokozana na kuhusudiana.
Wakolosai 1:29
Nami najitaabisha kwa neno lilo hilo, nikijitahidi kwa kadiri ya
kutenda kazi kwake atendaye kazi ndani yangu kwa nguvu.
Wafilipi 2:13
25
Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka
kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
1Korintho 12:11
lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule,
akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.
Roho Mtakatifu anapokuwa ndani ya mtu yule mtu
hawezi kujitukuza wala kujiona na uwezo wa kutenda kazi
zaidi ya wengine.
Zaburi 33:11
Shauri la Bwana lasimama milele, Makusudi ya moyo wake
vizazi na vizazi.
Roho mtakatifu hajipingi mwenyewe, anapoamua jambo
lifanyike katika yeye lazima lifanyike kama alivyoamua wala
hawezi kugeuka tena akasema nilikosea au hapana hili halipo
sawa hivyo fanya kivingine, bali yeye akisema moja leo na
kesho akija atasema ileile moja ya jana.
2Korintho 13:1
Hii ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya
mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.
Kila neno la Roho Mtakatifu ni muhimu kulipima kwa
kusubiri lithibitike kwa watu zaidi ya mmoja, au kwa kuomba
ishara ya kuhakikisha lile neno.
26
Wakolosai 3:15
Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa
katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.
Endapo utataka kufanya maamuzi fulani, angalia
kiwango chako cha imani halafu angalia amani iliyoko ndani
yako, usiangalie njia au mpenyo wa kufanya ila angalia amani
iliyo ndani yako.
Kwa sababu Roho Mtakatifu anakaa ndani yako basi
yeye atakuvuta na kutia msukumo mkubwa ndani yako,
pengine hata kwa machozi, na unapoamua kutokana na huo
msukumo ndani yako kuna mahali pa kuanzia kama utaanza na
hatua kuelekea kufanya ama kutoa maamuzi(starting point).
27
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
Sehemu ya tano
Roho mtakatifu anapokuwa ndani yako unakuwaje?
Utaichukia dhambi
1Yohana 3:6 na 9
Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi
hakumwona yeye, wala hakumtambua.
9Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu
uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa
sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
1Yohana 5:18
Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi;
bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu
hamgusi.
Kwako dhambi inakuwa ni kama jambo linalokereketa,
na lenye kukupoteza, hivyo unajikuta unaichukia dhambi sana,
wala huoni amani katika mazingira ya dhambi.
Unajawa na amani ya Kristo ndani yako.
1Korintho 14:33
Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile
vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.
28
Ndani yako hauoni jambo la kukukwaza, kila jambo
kwako ni kama maji yanayopita taratibu na kupotea kabisa,
huna shaka na maudhi yoyote kutoka kwa mtu yoyote bali ni
amani tu moyoni, hii inasababisha uchukuliane na watu wote
ilivyo sawa sawa. Ila sasa hapa wivu wa Bwana unajaa ndani
yako, mambo ambayo yataweza kukukwaza ni yale
yanayomtukanisha Kristo au Roho Mtakatifu.
Utapenda kusoma neno la Mungu mara kwa mara.
Luka 8:21
Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao
walisikiao neno la Mungu na kulifanya.
Ebrania 4:12
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali
kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata
kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani
yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
1Petro 1:23
Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo,
bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima,
lidumulo hata milele.
Utajikuta unafuraha zaidi unaposoma maandiko yenye
uzima, na kusikia mafundisho ya neno la Mungu kuliko kitu
chochote kile katika maisha yako.
29
Utapenda kuomba kila wakati.
Yuda 1:20
Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu
sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu,
Thesalonike 5:17
ombeni bila kukoma;
Mathayo 14:23
Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani
faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako
huko peke yake.
Matendo 6:4
na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.
Yakobo 5:16
Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate
kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba
kwa bidii.
Utamshuhudia Kristo kwa watu wengine.
Marko 16:15
Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili
kwa kila kiumbe.
30
Luka 9:6
Wakaenda, wakazunguka katika vijiji, wakihubiri injili, na
kupoza watu kila mahali.
Warumi 1:16
Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu
uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na
kwa Myunani pia.
Warumi 15:20
kadhalika nikijitahidi kuihubiri Injili, nisihubiri hapo ambapo
jina la Kristo limekwisha kutajwa, nisije nikajenga juu ya msingi
wa mtu mwingine;
1Korintho 9:18
Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa
Injili bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu
nilio nao katika Injili.
Shauku yako ni kuona watu wote wanamjua Kristo,
hivyo utajikuta unatabia ya kumshuhudia Kristo kwa mtu
yoyote mahali popote.
31
Utajawa na utendaji wa tunda la Roho
Wagalatia 5:22-25
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu
wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama
hayo hakuna sheria.24 Na hao walio wa Kristo Yesu
wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na
tamaa zake.25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
Ndani kunavutwa zaidi katika kuyatenda na kuyaona
mambo mema, na huu ndio uchaji hasa.
Utapenda kumwadhimisha Mungu maishani mwako.
Warumi 15:5-6
Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunia mamoja
ninyi kwa ninyi, kwa mfano wa Kristo Yesu; 6 ili kwa moyo
mmoja na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu, Baba
wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Ukikaa utajikuta unanena kwa lugha, au unamtukuza
Mungu, na maneno ya Mungu hayaishi kinywani mwako hata
ukiwa peke yako kwa mfano: asante Yesu, Mungu yupo,
Haleluya n.k.
32
Unajawa na hofu ya Mungu.
2Korintho 5:11
Basi tukiijua hofu ya Bwana, twawavuta wanadamu; lakini
tumedhihirishwa mbele za Mungu. Nami natumaini ya kuwa
tumedhihirishwa katika dhamiri zenu pia.
1Petro 3:2, na 15
wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 15 Mwe tayari
siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo
ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.
Ndani yako utajikuta hufanyi jambo kama zamani bila
kujali, hapana ndani yako utaona maamuzi yako yanajali sana
kama unamkosea Mungu au la, kila utakachofanya utajihoji
kwanza kama ni halali kwako kufanya hivyo au la.
Unakua katika imani.
Matendo 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu
huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye
imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.
Warumi 15:13
Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani
katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika
nguvu za Roho Mtakatifu.
33
Kila unachokifanya utakifanya kwa imani inayotokana
na neno la Mungu, hivyo kila wakati unajikuta unakua zaidi
kiimani na kujikuta roho yako inafanikiwa zaidi.
Unajaa nguvu za kiroho.
Warumi 15:18-19
Maana sitathubutu kutaja neno asilolitenda Kristo kwa kazi
yangu, Mataifa wapate kutii, kwa neno au kwa tendo,19 kwa
nguvu za ishara na maajabu, katika nguvu za Roho Mtakatifu;
hata ikawa tangu Yerusalemu, na kando kando yake, mpaka
Iliriko nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa utimilifu;
Kiwango chako cha nguvu za Mungu kinakua na
kuongezeka, utiisho wa kiungu unajaa ndani yako, maana yeye
atendaye kazi ndani yako ndiye mwenmye sehemu ya nguvu
iliyopo ndani mwako. Na hizi nguvu ndizo zinazoitwa zawadi
za Roho Mtakatifu au Karama za Roho Mtakatifu.
34
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
Sehemu ya sita
Karama za Roho Mtakatifu.
Hizi ni karama ambazo zinajulikana pia kama karama za
rohoni. 1Korintho 14:1.
Juu ya karama za rohoni, tunamafundisho kadha wa
kadha tunayoweza kuyaona kupitia neno la Mungu Biblia,
lakini tunajifunza kutoka katika sehemu tatu tu katika Biblia.
Warumi
12 inazungumzia juu ya karama hizi,
1Wakorintho sura ya 12 na 14 pia zinazungumzia juu ya hizi
karama, na tena katika Waefeso 4:7 inazungumzia hizi karama
za Roho Mtakatifu ama karama za Rohoni.
Mungu kupitia watumishi wake aliowapa neema ya
kuandika kwa ajili yetu anakusudio la kututaka tujue kuwa kila
utendaji wa kazi katika kanisa leo tunahitaji karama za Roho
Mtakatifu ili tufanikiwe kutimiza kila makusudi yake
aliyoyakusudia katika maisha yetu.
Tunapoanza kuziangalia hizi karama kwanza tujue
karama ni kitu gani ili tutakapoanzakuziangalia utendaji wake
tuwe tumajua maana na ni kitu gani.
Karama ni nini?
Ni kitu kinachotolewa na Mungu kupitia roho Mtakatifu ili
kuuhudumia mwili wa Kristo ambao ndio kanisa. 1Korintho
12:7 na 27,
35
Hizi karama zinatolewa kwa kufaidiana, (iwe mfaida
wengine). 1Korintho 12:7 na 27, 7Lakini kila mmoja hupewa
ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
17-18 Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama
wote ni sikio ku wapi kunusa? Bali Mungu amevitia viungo kila
kimoja katika mwili kama alivyotaka.
Kwa nini ziitwe karama?
Lugha ya hili neno inatafsiriwa kutoka kwenye lugha ya
kigiriki ambayo ni "karismaton" ambayo inamaana ya zawadi
kwa "kiswahili" na kimombo ni "gift".
Hivyo kwa wagiriki walipokuwa wakitoa zawadi
waliziweka katika mafungu mawili, fungu la kwanza ni zawadi
anazopewa mtu kutokana na kazi aliyoifanya na zawadi
anazopewa mtu asizostahili ambazo hasa ndizo zinazoitwa
"Karismaton" kwa kigiriki.
Mtu anapokea zawadi hizi akiwa tayari amemkiri Yesu
kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake; hivyo huja baada ya
Yesu kuingia ndani ya mtu.
Na mara baada ya kupokea karama hizi, hazimwondoi
Yesu katika maisha ya mtu huyo, Yesu anashika namba moja
ndipo karama zifuatie, hivyo mtu mwenye hizi karama
anamuhesabu Yesu ndiye mwanzilishi wa karama hizi, na
ndiye kichwa cha kanisa na yeye huyo mtu anajihesabu ni
mwili wa Kristo ama kanisa(hekalu).
Kwa hiyo bila Yesu hakuna karama za Roho, na bila
karama za Roho hakuna uwezo wa kutenda kazi za Yesu.
36
Matendo 1:4 Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza
wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo
mlisikia habari zake kwangu;
Yesu anawaambia wale tenashara wasitoke mpaka
waipokee ile ahadi ya kuwaletea msaidizi mwingine ambaye ni
Roho Mtakatifu, alijua kama watatoka na kwenda kufanya kazi
hawataweza kabisa kwa ufahamu wao wa kibinadamu, hivyo
walihitaji zaidi ufahamu wa kiungu ndani yao ili waweze
kufanya yote aliyowaamuru, na njia pekee ya kufanya kwa
uwezo wa kiungu ni kungoja wajazwe na Roho Mtakatifu;
utaona baada ya kujazwa na Roho Mtakatifu ndipo walipoweza
kupata ujasiri wa kuhubiri injili, na kufanya zile kazi ambazo
Yesu alizitenda.
Karama za rohoni zinamfanya muumini kutenda kazi
alizozitenda Yesu na zaidi ya zile alizozitenda.
Yohana 14:12
Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi
nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko
hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.
Warumi 12:5-8
Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na
viungo, kila mmoja kwa mwenzake. Basi kwa kuwa tuna karama
zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii,
tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika
huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;
mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa
37
moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye
kurehemu, kwa furaha.
Tuziangalie hizi karama ni zipi?
1Korintho 12:4-11
1.
Neno la hekima
Hizi ni karama zinazoongozwa na maneno au maamuzi sahihi,
kwa wakati sahihi, na kwa mahali sahihi, lakini sawasawa na
maandiko yanavyosema.
1Korintho 2:12,13 inasema, Lakini sisi hatukuipokea roho ya
dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua
tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno
yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali
yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa
maneno ya rohoni.
Mtu hawezi kufanya au kunena maneno yanayotoka kwa Mungu
isipokuwa kwa kupewa na Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu,
na hakuna hekima inayopita hekima zote kama si hekima ya
Kiungu inayotolewa na Roho Mtakatifu.
Kwa kigiriki neno hekima ni "sofia"
Hekima ni mtu kusema, kufanya na kutenda jambo sahihi kwa
watu sahihi, mahali sahihi, kwa muda sahihi na kwa lugha
sahihi.
38
2.
Karama ya maarifa (gnosis)
Hii ni karama inayohusika katika namna ya kutatua
changamoto fulani, kuongoza watu fulani ama kubuni jambo
litakalokuwa ni msaada kwa kanisa, lakini kila ubunifu wake
unaongozwa na neno la Mungu kutoka katika maandiko
matakatifu.
1Korintho 12:8
Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na
mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;
1Korintho 13:2a
Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote,
……….
Hivyo mtu mwenye hii karama hakaukiwi maarifa kinywani
mwake, na hata katika kila atakachokifanya kitakuwa katika
maarifa ya Mungu.
3.
Karama ya Imani
Kila mtu anapaswa kuwa na imani sawa na neno la Mungu
katika Waebrania 11:6 linsema, Lakini pasipo imani
haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu
lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu
wale wamtafutao.
Acha imani hii ya ujumla wa kila mtu awe nayo lakini
mbali na hii kuna ile ambayo anapewa mtu kama karama ndani
yake ili kuwa msaada kwa kanisa,na hii imani inakuwa ni ile
iliyozidi kawaida ya mwanadamu.
39
Imani hii inatumika kupitisha mambo ambayo
yanaonekana hayapiti katika uwezo wa kawaida, kutia moyo
mahali ambapo kunakuvunjika moyo, na kuvusha watu toka
katika kila hali ya mateso au changamoto fulani.
Karama hii inaweza kulifanya kanisa kuwa na matumaini ya
ushindi wakati wote, hivyo ndani ya kanisa ni lazima kuomba
sana kuwa na aina hii ya karama.
1Korintho 12:1-9a
Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose
kufahamu.2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa,
mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa.
3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika
Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu
kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. 4
Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. 5 Tena
pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. 6 Kisha pana
tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi
zote katika wote. 7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho
kwa kufaidiana. 8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la
hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye
yule; 9mwingine imani katika Roho yeye yule;
4.
Karama ya uponyaji
Hii karama ni ya muhimu sana katika kulitangaza jina la Yesu
Kristo, na mahali penye aina hii ya karama watu wengi
wanakimbilia, kwasababu watu wengi wanatamani kuishi
wakiwa na afya bora pasipo magonjwa. Lakini magonjwa ni
sehemu ya mateso kwa mwanadamu, hata hivyo si lazima
40
mpaka hii karama tu ndipo watu waponywe magonjwa,
hapana, isipokuwa uponyaji ni wa namna apendavyo Mungu.
1Korintho 12:1-2,7-9
Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose
kufahamu. 2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa,
mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa.
7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. 8
Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na
mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;
9mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama
za kuponya katika Roho yule mmoja;
Tunasema hii ni karama ya muhimu kwa sababu
karama ni zawadi pasipo kustahili, hivyo ni kitu kinachoishi
ndani ya mtu, sasa uponyaji ukiwa unaishi ndani ya mtu moja
kwa moja mtu huyo atakuwa mara kwa mara amejikita zaidi
kwenye maswala ya uponyaji, mfano: kujaribu kumgusa mtoto
kichwa na kujua jotoridi la mwili na kumpatia dawa ya
maumivu kisha mtoto kupona maumivu ya kichwa haimaanishi
wewe ni daktari(mganga), bali utakapoonana na daktari
atakueleza maelezo yanayoweza kukusaidia zaidi katika hilo
jambo, yeye atatumia vipimo na kugundua aina ya ugonjwa na
kumpatia dawa inayostahili wala siyo tu hiyo ya kutuliza
maumivu. Hii niifananishe na hiyo karama ya uponyaji,
haihusishi kutuliza tu bali inasababisha tiba kabisa kwa
mgonjwa au mkwa mwenye changamoto, uponyaji huu
unaweza kuwa ni wa nafsi, au mwili ama roho. Sasa haijalishi
kuna mtumishi ameweka mikono kwa mgonjwa mara Yule
mgonjwa akapona ndio ikawa ni kipimo cha kuwa na karama
41
ya uponyaji la hasha, tuangalie habari za Anania na Sauli
ambaye baadaye aliitwa Paulo….
Matendo 9:12-15
naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea
mikono juu yake, apate kuona tena. Lakini Anania akajibu,
Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya
mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu; hata hapa
ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote
wakuitiao Jina lako. Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa
maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu
mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli.
Hili fungu linaonesha namna Mungu anavyoweza
kumtumia mtu kuponya hata kama hiyo siyo karama yake,
yeye anaponya mara moja kwa ajili ya kusudi la Mungu.
Ukilinganisha na mtu mwenye karama ya kuponya
ambayo hata nguo zake zinatembea na upako huo wa
kuponya.Amewekewa zawadi ndani yake na kila wakati hata
kama yeye hajui juu ya mgonjwa katika kundi lakini
anapoonekana tu mgonjwa anaweza kupona, tazama hili fungu
katika Biblia:
Matendo 19.12
hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini
mwake, magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu
wakawatoka.
Paulo anaponya kwa uweza wa Mungu wala si kwa
uweza wake wala si kwa nguvu zake ila nguvu hiyo ipo ndani
42
yake, hivyo yeye anatumika kama chombo cha kuhifadhia
uponyaji tu wala uponyaji sio wake.
Matendo 9.34
Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka,
ujitandikie. Mara akaondoka.
Hapa ni kwa nini aseme Yesu akuponya ikiwa yeye
Petro ndiye yupo pale na Yesu haonekani pale? Jibu rahisi ni
kwamba Petro anaishi ndani yake Yesu na Yesu anaishi ndani
yake Petro, hata kile akifanyacho Petro ni matokeo ya kile
alichokifanya Yesu ndani yake.
5.
Karama ya miujiza
Kwani umewahi kuona au kusikia wahubiri wanapokuja
kwenu kila siku Mungu anajifunua kwa namna tofauti na
kuwatumia wahubiri kuponya na kufungua papo hapo? Miujiza
ni kitu cha ajabu kinachotokea bila kutegemea papo hapo, hapa
hausubiri kesho ni jambo linalofanyika ana kwa ana.
1Korintho 12:7-10a
7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. 8
Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na
mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;
9mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama
za kuponya katika Roho yule mmoja;10na mwingine matendo ya
miujiza;
43
Huu ni uweza wa Mungu ndani ya mtu ili Mungu ajifunue kuwa
yupo mahali pale na watu wapate kumwamini Yesu.
Matendo 9.33-35
Akamwona mtu mmoja huko, jina lake Ainea, mtu huyo amelala
kitandani miaka minane; maana alikuwa amepooza. Petro
akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie.
Mara akaondoka. Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni
wakamwona, wakamgeukia Bwana.
Tunaona mara baada ya Ainea kupokea muujiza watu
wote wanamgeukia Bwana, hivyo kusudi kubwa la muujiza ni
ili watu wamtambue Yesu Kristo anayehubiriwa mahali pale.
6.
Karama za unabii
Hizi ni aina za karama ambazo Roho Mtakatifu anamtumia mtu
katika maeneo matatu, moyo, macho na kinywa. Mtu aliyepewa
hizi karama anajulikana kama nabii, hapo mwanzo nabii
aliitwa mwonaji
1Samweli 9:9 (Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda
kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa
mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa
Mwonaji.)
Mwonaji ni macho ya Mungu, na ni kinywa cha Mungu pia,
hivyo nabii ni kinywa cha Mungu na ni macho ya Mungu.
Huyu mtu (nabii) huzungumza na Mungu na kusema na watu
wa Mungu juu ya yale aliyozungumza naye, naye huwa kama
mtu aliyetumwa, wala hazungumzi kwa mamlaka kanakwamba
44
yanatoka kwake, isipokuwa anazungumza kama mtu
aliyetumiwa na Mungu kuzungumza, kwa mfano: “Bwana
asema” ndiyo hasa anavyoanza au kumaliza ujumbe wake.
Na nabii hutoa unabii ili kulijenga kanisa wala si vinginevyo,
pia nabii ni mtu aliyechini ya mchungaji maana naye inampasa
kuchungwa chini ya mchungaji tutamuelezea nabii zaidi katika
zile huduma tano za kanisa.
Basi karama hii ya unabii inatumiwa na Mungu kuzungumza na
kanisa ndani ya kanisa kwa lengo la kulijenga kanisa. Mtu
mwenye hii karama anaona na kusikia mambo au maelekezo
ya Mungu kwa kanisa.
7.
Karama za kupambanua roho
Ndani ya kanisa kunakuwa na muingiliano mwingi sana wa
kiroho, na ukizingatia haya mambo ya rohoni yanahitaji
muongozo sahihi katika kuyafanya na kukubaliana nayo,
shetani ni roho na Mungu ni roho isipokuwa tofauti yao ni
kwamba Mungu ndiye chanzo cha mambo yote
tunayoyafahamu hapa ulimwenguni mfano elimu, pesa, madini,
ndoa, uzao, sheria na siasa, lakini shetani ni mfuatiliaji tu wa
mambo yote tunayoyajua, katika kufuatilia, yeye kwa kuwa ana
uadui na wana wa Mungu hivyo anatumia hila nyingi
kuhakikisha wana wa Mungu wanapotea njia sahihi ya
kumwabudu Mungu na kumfuata Mungu, hivyo atatumia
ulimwengu wa roho kupotosha, na ndiyo maana sasa tunahitaji
sana hii karama ya kupambanua roho ili tuzifahamu hila za
adui ndani ya kanisa.
Isaya 21:2
45
Nimeonyeshwa maono magumu; atendaye hila anatenda hila,
mharibu anaharibu. Panda juu, Ee Elamu; husuru, Ee Umedi;
mimi ninakomesha maombolezo yake yote.
Hii karama inasaidia kumjua roho yupi atendaye kazi ndani ya
kanisa, ikiwa kunauvamizi wowote wa kipepo ndani ya kanisa
tukiwa nah ii karama tutautambua haraka kabla haujaleta
madhara kwa kanisa.
8.
Karama za aina za lugha
Hizi ni aina za karama ambazo zinahusisha ulimi na
matamko. Karama hizi zipo katika mafungu mawili: i) lugha za
wanadamu, ii) lugha za malaika; katika hizi aina za karama
mtu anayepewa hizi karama huwa anajikuta akizungumza aina
mbalimbali za lugha za wanadamu au lugha za malaika pasipo
kwenda chuo wala shule ya lugha. Lugha za wanadamu ni
lugha zinazozungumzwa na makabila au mataifa mbalimbali,
mfano Kiingereza, Kiswahili, au Kichina, ama lugha zingine
zinazojulikana na watu wa hiyo lugha. Matendo 2:2-9 Kukaja
ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu
ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
3Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto
uliowakalia kila mmoja wao. 4 Wote wakajazwa Roho
Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho
alivyowajalia kutamka. 5 Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi
wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6
Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa
na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa
lugha yake mwenyewe. 7 Wakashangaa wote, wakastaajabu
wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8
Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa
46
nayo? 9 Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao
Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia,
Bila shaka umeona hizi lugha walizokuwa wakinena,
lakini hakikuwashangaza kusikia wakikinena hizo lugha bali
kilichowashangaza ni pale waliposikia wakinena lugha za watu
wa mataifa mbalimbali ikiwa wao ni taifa jingine ambapo
hawakuwahi kuzungumza hapo kabla.
Sasa mtu anaponena kwa hii lugha ya wanadamu basi
aweze kuwepo na mfasiri ili kutafsiri yale yanayosemwa hapo,
ili watu wasioijua hiyo lugha waweze kuelewa kile ambacho
Roho Mtakatifu anasema; hapo ndipo tunapoweza kusema ni
bora kukaa kimya kuliko kunena kwa hii lugha ikiwa hakuna
anayeweza kutoa tafsiri ya hiyo lugha, kwa mfano katika fungu
la hapo juu la Matendo ya Mitume 2:2-9 watu waliokuwepo nje
ya lile jengo waliposikia walishangaa kusikiwa wakinena lugha
za mataifa yao, hivyo ni vizuri kama wanaosikiliza wakaelewa
maana ya yale unayonena la sivyo hakuna sababu ya kunena
kwa lugha za wanadamu mbele yao.
1Korintho 14:27-28 Kama mtu akinena kwa lugha, wanene
wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na
mmoja na afasiri.Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na
anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena
na Mungu.
Lakini mtu anaponena kwa lugha za malaika ndipo
tunapoesama mtu huyu anazungumza na Mungu na lengo
kubwa la Roho Mtakatifu ni kumjenga huyo mtu anayenena hii
lugha wala hata yeye hajui kile anachokizungumza wakati huo
bali anaijenga nafsi yake. 1Korintho14:2-5 Maana yeye
47
anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu;
maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho
yake. 3 Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya
kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo. 4 Yeye anenaye
kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa.
5 Nami nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini zaidi sana
mpate kuhutubu, maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye
anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili kusudi kanisa lipate
kujengwa.
Kunena kwa lugha hii ni vizuri sana wala hapana
masharti unapokuwa ukinena kwa hii lugha ili mradi uwe
kweli katika Roho, japo kama utahutubu (utafundisha)ni vizuri
zaidi ya kunena ili mtu asiyefahamu mambo ya Roho Mtakatifu
aweze kuyafahamu yale unayosema.
NB: 14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini
akili zangu hazina matunda. 15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa
roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena
nitaimba kwa akili pia.
Mtu anayenena kwa lugha anaweza kukumbuka,
anaweza kujitambua mahali alipo, anaweza kujijua na
kijitawala wala hawezi kupoteza ufahamu wake kwa sababu ya
kuzama katika maombi, isipokuwa atazama katika maombi bila
kuyahisi mambo ya mwilini mfano uchovu, njaa, au mambo ya
mwilini yanayoshindana na roho yake. Hivyo mtu akinena
halafu hawezi kujitawala huyo atakuwa amevamiwa na pepo
wala siyo Roho Mtakatifu.
9.
Karama za tafsiri za lugha
48
Hizi ni karama zinazotegemea kusikia na kuzungumza
kile unachokisikia kwa kutoa ufafanuzi zaidi kutoka kwenye
maneno uliyoyasikia kwa mtu anayenena kwa lugha ngeni,
1Korintho 14:12-15
Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu
wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili
kulijenga kanisa. 13 Kwa sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha
na aombe apewe kufasiri.
1 Wakorintho 12 : 1-31
Utendaji wa Karama za rohoni hautufikishi kukutana na
Mungu na kutufikisha Mbinguni ni kwa ajili ya kulijenga
kanisa pekee(mioyo na nafsi au kusanyiko la watu wa
mahali pamoja).
1Korintho 13:2
Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote,
nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha
milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
Hili fungu linazungumzia utendaji wa karama hizi;
karama zote haziwezi kumfanya mtu akawa kitu mbele za
Mungu, isipokuwa akiwa na hizi karama basi awe na upendo.
Upendo wa kweli unaomfanya Mungu kuwa wa kwanza na
kuwafanya watu kuwa wa pili halafu wewe mwenyewe kuwa
wa mwisho katika kujali na kuhudumu.
49
Sifa za upendo wa kweli
1Korintho 13:4-8
Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo
hautakabari; haujivuni; 5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti
mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6
haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7
huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii
utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa,
yatabatilika.
Katika hizi karama za rohoni tunaweza kuzipata kwa kuzihitaji
na kumwambia Mungu atoaye karama atujalie na sisi tuweze
kuwa nazo, lakini hutuwi nazo ili zitusaidie katika mambo yetu
binafsi bali ili kuujenga mwili wa Kristo (Kanisa kama watu
wanaomtafuta Kristo katika kutaniko moja).
Bila shaka ulipomaliza kukisoma hiki kitabu kuna mambo
mazuri umeyafurahia sana ambayo utayatendea kazi, naomba
nikupe angalizo, usiache kukusanyika kama ilivyo desturi, ili
kama yamkini utaendelea kujazwa na Roho Mtakatifu kila siku
na kila wakati, maana ujazo wa Roho Mtakatifu unaendelea kila
siku , kila muda, na kila mahali, ambapo wewe unatakiwa uwe
umejazwa na uzidi kujazwa, kila unapojazwa na Roho
Mtakatifu unapelekwa kwenye kiwango kingine cha kiroho.
Ukitaka ufanikiwe sana katika kila kitu lazima uwe umejazwa
na Roho Mtakatifu kila wakati, maana yeye nndiye
50
anayetupeleka katika kweli yote. Mtu aliyejazwa na Roho
Mtakatifu anauwezo wa kushinda dhambi hata kama ni dhambi
ya namna gani lazima Roho Mtakatifu atamkumbusha sawa
sawa na neno lake.
Mungu akubariki sana kwa kusoma kitabu hiki, na ni imani
yangu kuwa umefunguliwa sana na kubarikiwa sana na jumbe
za kitabu hiki, Amina Utukufu.
+255 762 282777, na +255 718 613491
revmwakifwamba@gmail.com
51
MWISHO
ROHO MTAKATIFU KATIKA KANISA
Kimeandikwa na:
Rev Anthony Mwakifwamba
+255 762 282 777 na +255 718 613 491
P.O. BOX 2256, Dodoma City, Tanzania
Na kuchapishwa na
Copyright ©2019
Haki zote zimehifadhiwa hauruhusiwi
kunakili, kunukulu wala kuchapisha maneno
ya kitabu hiki kwa lengo la kuuza kitabu hiki
bila idhini ya mwandishi.
52
Download