Uploaded by faith.shimba

Habakuki

advertisement
Kitabu Cha Habakuki
Mwandishi: Habakuki
Mwaka: kati ya 612 -589 Kabla ya Kuzaliwa Kristo
Wahusika wakuu: Habakuki na Wakaldayo
Yaliyomo:
1. Swali la Habakuki na Jibu la Mungu, Sura 1:1—1:11
2. Swali la Pili la Habakuki na Jibu la Mungu Sura 1:12 – 2:20
3. Maombi ya Habakuki, Sura 3
Maana ya Jina Habakuki
Habakuki, ambaye maana yake ni “kumbatia” au “mshindani mweleka”. Mwandishi wa kitabu
hiki haelezi maisha yake binafsi na hataji kwa uwazi mwaka alipotoa ujumbe. Habakuki alikuwa
nabii wa Yuda kutoka kabila ya Lawi. Alikuwa ni mmoja wa waimbaji wa hekaluni.
Maudhui ya Kitabu hiki:
Kitabu hiki kimeandikwa kwa mtindo wa mazungumzo kati ya Mung una nabii (Habakuki).
Kitabu hiki kinazungumzia suala la mateso, dhambi na haki ya Mungu kama ilivyo kwa
Ayubu na Zaburi ya 73.
Nabii Habakuki katika Mazungumzo yake na Mungu, anaonyesha kushindwa kwake kuelewa ni
kwa jinsi gani Mungu angeweza kuwatumia Wakaldayo, taifa ovu kuliko wayahudi (Israeli)
kutekeleza hukumu ya Mungu juu ya taifa la Israeli, taifa lililokuwa limechaguliwa na Mungu.
Habakuki anaanza kwa kumlalamikia Mungu kuwa Yuda hakutekeleza ujumbe aliopewa.
Anauliza, hadi lini Yuda waendelee katika uovu bila kuadhibiwa. Mungu anajibu kuwa anaandaa
adhabu itakayotolewa kwa kutumia Wakaldayo (Wababeli).
Habakuki anabisha mpango huo akisema: kama Mungu ni Mtakatifu na wa haki, na Wayahudi ni
watu wake itawezekanaje Wakaldayo wenye maovu mengi kuliko Wayahudi (Israeli) watumiwe
na Mungu? Jibu la Mungu ni kuwa kila dhambi huleta hukumu. Hivyo wote watapata adhabu ya
uovu wao. Mungu pia anamwambia Habakuki Mwenye haki ataishi kwa Imani, na Kwamba
wanapaswa kuwa na uhakika ya kwamba Mungu alikuwa anafanya lililo sahihi kuwatumia
wakaldayo walio waovu kutekeleza hukumu au adhabu yake kwa wana wa Israeli waliokuwa ni
taifa teule. Pamoja na Hayo Mungu anamwambia Habakuki, Muda si mrefu wakldayo nao
wangepata hukumu yao.
Ujumbe Wa kitabu hiki:
Ujumbe wa Habakuki ni BWANA Mungu sio Mungu wa Israeli na Yuda tu, yeye ni Mungu wa
ulimwengu wote. Yuda na Kaldayo (Babeli) wataadhibiwa kwa kufuata maovu yao. Vile vile
amtegemeaye Mungu akawa mwadilifu hana haja ya kuogopa hukumu maana “Mwenye haki
ataishi kwa Imani”. Mungu atampa ushindi (2:4).
Kusudi la Ujumbe wa Kitabu hiki
Ni kuonyesha kwamba, Mungu ndiye nayeitawala dunia. Hata kama tunaona uovu na maovu
yakiongezeka sana, Hata hivyo Mungu ataadhibu uovu na waovu siku moja na kuutowesha
usiwepo tena.
Wazo kuu la Kitabu hiki
Mungu anaweza kutumia yeyote hata waovu kuadhibu watu wake walioitwa kwa jina lake
wanapokwenda kinyume na maagizo yake; nia ikiwa ni kuwakumbusha na kuwarudisha watu
wake katika njia sahihi. Hata hivyo, waovu hawa wakiisha kutimiza kusudi la Mungu nao
huadhibiwa kwa uovu wao.
Mambo Muhimu
1. Mungu hutumia waovu kuwaadhibu watu wake wanapokosea
2. Imani na Mamlaka ya Mungu yanatupa uhakika ya kwamba Mungu ana haki katika njia
zake zote.
Download