SURA YA 5

advertisement
IJUMAA
Ijumaa ilianza bila ya mbwembwe. Niliamka nikiwa na tamaa
ya kuwa mikononi na katika sita kwa sita ya aina yake na
Freddy Mjamaika wangu toka Uluguru. Katika mawazo yangu
na hisia zangu zote Freddy alikuwa ni Mjamaika daima kwani
hata Kiswahili chake bado kina lafudhi kali ya Kijamaika.
Hivyo niliamka nikiwa na matamanio ya ajabu. Unajua kuna
wakati wanawake tunaamka asubuhi ukiwa na hamu ya
kufanya mapenzi ambayo mfano wake hakuna, ni hamu
ambayo inapenya kwenye mifupa na mishipa, inaacha alama
kwenye chembechembe za damu na endapo unapata nafasi ya
kupata cha kuamkia basi kinakuwa cha kutiana kucha na
kuumana meno. Hivyo ndivyo nilivyo amka asubuhi ya Ijumaa.
Nilitamani kile alichokianzisha jana pale Blue Pearl
angekimalizia kuanzia asubuhi ile. Uzuri nikuwa kuliko ilivyo
kawaida Waziri aliondoka mapema kwa ajili ya kusimamia
maandalizi ya mwisho ya sherehe za Muungano kesho yake.
Nilimaliza mambo ya hapo nyumbani kama kwenye saa tatu
hivi nikawa nimedhamiria ikifika saa tano niwe ninaondoka
hapo kuelekea Saloon. Nilikuwa na miadi kule ya saa nane za
mchana. . Sijui kitu gani kilikuwa kimenishikilia kwani
nilijisikia hamu ya kumtumia Freddy sms ya kumjulia hali au
nifanye tu ili niweze kuwasiliana naye. Ningeweza kumpigia
hata hivyo niliamua kumtumia ujumbe mfupi wa simu:
Mimi:Mambo Freddy, za asubuhi!
Haikuchukua muda mrefu nikapata majibu yake. Moyo
uliniruka kwa furaha. Nilikuwa kama mtoto wa sekondari
aliyepata ujumbe toka kwa rafiki yake wa kiume. Niliacha
mambo mengine nikaenda kukaa sebuleni.
Tukaanza
kuandikiana jumbe fupi fupi – angalau kwa mawazo yangu.
Yeye: Hi Clementina! how are you?
Mimi: I’m fine, thank you. How about you?
Yeye: I’m better now. Mambo vipi darling?
Kusoma hilo neno “darling” kwenye simu yangu nilijisikia
furaha. Nilijisikia nahitajiwa na ninapendwa.
Mimi: Pouwa tu, nasikia raha yaani umechukua muda kuwa na
mimi.
Yeye: Mambo mengine nafikiri njama zinafanyika mbinguni!
Mimi mwenyewe nimefurahi wewe kunitafuta na kunipata.
Milele nitashukuru.
Huyu kijana alikuwa ni mjuzi wa maneno; alikuwa anajua
kuyapanga na yakaa vizuri kama Ukuta Mkuu wa China.
Niliona raha moyoni. Tukaendelea kubadilishana sms kwa
muda kidogo.
Yeye: Nimebakia kujiuliza ulikuwa wapi muda wote wa
maisha yangu Clementina?
Mimi: mhh.... sijui nilikuwa wapi..au labda tuseme..wewe ndio
ulikuwa umejificha wapi siku zote?
Nilijicheka kidogo. Niliendelea kumuandikia. Muda huo
niliweza kusikia sauti ya magari yakipita si mbali sana na
nyumbani na watumishi walikuwa wakifanya shughuli zao na
mtumishi wetu wa ndani alikuwa akifanya shughuli za usafi.
Niliona hapo sebuleni hapafai nikaamua kupanda gorofani
chumbani ili niwe katika faragha yangu, maana kijoto kilianza
kunipanda
taratibu.
Mimi: sijui hata nikuambie nini mpenzi Freddy, nadhani
tukubali kuwa kila kitu kina muda wake..na muda ndio
umewadia
Yeye:: Lazima nikiri Clementina kuwa japo kule kunigonga
niliona ni mojawapo ya mikosi mikubwa kunikuta maishani na
niliilaani siku ile lakini sasa naamini yawezekana ile ilikuwa ni
mpango tu wa Jah kukuleta wewe maishani mwangu,
Namshukuru Jah Rastafari!
Nilitamani kucheka kwa sababu huyo Jah miye ndiye nilikuwa
namsikia kwake. Na kama kweli huyo Jah ndiye anafanya
mambo kama haya basi na mimi niko tayari kumuunga mkono!
M: Usinikumbushe tena siku ile dear, ilikuwa moja ya siku
ngumu sana kwangu....sijui hata niliingiwa na nini hadi
nikakukosea heshima kiasi kile.....please usikumbushie tena
tafadhali.
Y: Kwangu ni siku ya kukumbuka milele siwezi kuisahau
kwani ni kama chungu-tamu, na nakuomba usiisahau kwani
tutakaa tucheke kila tukiikumbuka. Nakusihi usijisikie tena
vibaya kwani ulichodhania ni kibaya yawezekana kimerudi
kuwa chema!
M: Huenda uko sahihi..lakini.......anyway basi ibakie utakavyo
japo najisikia mkosaji sana
Y: Kwanini tena na wakati umeshaniomba msamaha na
nimekubali na daima sitashikilia siku ile dhidi yako. Nataka
ufurahi kuwa nami, Tina.
Nilifurahia alivyoniita “Tina”.
M: Ok dear.... asante sana kwa kunisamehe...
Y: Unafanya nini Ijumaa hii au Daktari ndio kakubana?
M: Ijumaa..... sijapanga chochote bado... si unajua toka siku
ile..nimekuwa kama nimechanganyikiwa vile na kama
nisingefanikiwa kukuona ingekuwa vipi. Labda ingekuwa ni
kama deni ambalo anayetakiwa kulipwa haonekani.
Y: Niambie ingekuwaje darling?
M: Sitaki hata kufikiria maana huenda ningefanya kitu
ambacho kingeshangaza walimwengu!
Y: Like what dear? I'm interested to know now.
M: Mhhh..you may not like what I would have done hahaha
huenda ningetafuta watu wakusake wakuteke nyara... hahaha.
Love can make you go crazy unamkumbuka yule kijana aliyem
shoot rais au sijui ni pope kisa alikuwa anampenda Brooke
Shields miaka ya nyuma kidogo?
Y: Duh.. ndio ile ilikuwa tradegy! Lakini kwa kweli ungefanya
hivyo sijui ingekuwaje lakini nitafurahi milele kwani uliamua
kunitafuta. Hivi uliponikosa pale ulijisikiaje? lol
M: nilijiskia kuishiwa nguvu lakini moyo ukaniambia dont give
up; nikapata nguvu mpya.
Muda ukapita kidogo bila kupokea majibu yake. Nikawa na
wasiwasi nini kimemkuta au nimesema kitu gani kibaya.
Nikaanza kuingiwa na wasiwasi. Nikamtumia ujumbe
mwingine.
M: Mbona umekuwa kimya ghafla Freddy, umekumbuka nini?
Y: Hapana nilitingwa kidogo hapa usiwe na wasiwasi. Unajua
nakumbuka kama kwenye movie ulivyotokea pale hotelini
jana, nikilinganisha na ulivyonigonga utadhani ni tofauti ya
mbingu na nchi!
M: Hahahah...kwanini unasema hivyo?
Y: Ni kama nimewaona watu wawili tofauti! - sura yako ya
hasira na ghadhabu na sura yako ya ucheshi na upendo ni kama
sura za watu wawili tofauti kabisa. Sijui uliamkia upande gani
ile Jumatatu? LOL
M: Kweli mtu kabla hujafahamiana naye kwa karibu
usimhukumu hata mimi siku ile nilikuona tofauti kabisa.
Sidhani nilivyokuona ningetegemea hata siku moja kuwa
tungeweza kuwa tumekaa pamoja na kufanya yale
tuliyoyafanya jana.
Nilijisikia aibu kufikiria maana katika maisha yangu yote
sijawahi kufanya kitu cha kuthubutu kama kile. Yaani
kumuacha mtu anichezee kwenye mazingira kama hayo na tena
nikafurahia hata sielewi kama ni jinni mahaba ndio limenishika
au ndio mwanzo wa mtu mzima kurukwa na akili.
Y: Teh teh teh niambie ulinionaje aada ya kunibamiza hadi
nikasikia kizunguzungu mwenzio?
M: Nilikuona kama mmoja wa wahuni wa mjini. Si unajua tena
.... ila kuna kitu kilinigusa...wakati nakufokea... ulivyokaa
kimya na kunitazama machoni..macho yako yalinifanya nisikie
kuchomeka moyoni kiana..nikaona upande wako mwingine
Freddy, mtu mwenye utu...sikustahili kukushushia maneno yale
hata kidogo. Na niliporudi nyumbani ile pica ikazidi kujirudia
ikaniingia akilini, mawazoni hadi nikajikuta nakuwazia zaidi
ya nilivyopaswa.kweli nilisikia aibu lakini.....basi!
Y: hahahahaha
M: Usicheke Freddy!
Y: Pole nacheka kwa sababu umesema uliniwaza usivyopasa!;
uliwaza nini?
Kwa sekunde chache nilitaka kumsimulia jioni ile ya kujipa
raha. Nilitaka kumuelezea kila fikra chafu na kila mguso wa
mahaba niliojipa mwenyewe. Natamani ningemwambia
kumuelezea kwa kina.
M: mhhhh! we acha tu maana.. kweli hata siku moja NEVER
SAY NEVER! litakapokupata la kukupata ndipo utajishangaa
kama ninavyojishangaa mimi sasa..
kwa mara ya kwanza katika maisha yangu... nilitafakari maana
ya utu...
Y: Kusema kweli nilichokiona machoni mwako siku ile
ilikuwa ni uchungu. Nilikuwa na uhakika mmoja kuwa
nilikuwa naadhibiwa kwa makosa ya mwingine, sijui huko
ulikokuwa unatoka kuna mtu alikutibua au nini lakini macho
yalijaa uchungu kweli!
M: Utu siyo kitu wala vitu kama ulijua....lakini labda tuyaache
hayo tuongee yetu mimi na wewe..
Y: Hamna neno siku moja labda utaniambia kwani natamani
nikufariji na kukufanya ujisikie kupendwa na kuthaminiwa
mpenzi.
M: Asante Freddy, kumbe uko mwelewa kiasi hiki pia?!
Nitakupenda
zaidi
kwa
hili...maisha
yanachekesha
sana..hivi..duniani kuna furaha ya kweli? wewe unafikiria je?
Sijui hata kwanini nilimuuliza juu ya jambo hilo. Mawazo
yangu yalikuwa yanazama sana katika maisha ya mbeleni
lakini wakati huo huo nilikuwa nimejikuta nimenaswa katika
mtego ambao umeniletea furaha katika namna na jinsi ambayo
kamwe sikuitarajia. Kumbuka ni mke wa waziri mimi!
Y: Naamini furaha ipo hasa ukiruhusu uipate kwani maisha
yana vizuizi vingi sana vya kuzuia watu kupata furaha!
M: Kwa mfano vitu gani hivyo vyenye kuzuia furaha?
Y: Vitu kama maumivu ya moyo, machungu ya maisha, na
mambo ambayo watu wengine hufanya dhidi yetu huharibu
uwezekano wa mtu kupata furaha. Na hii ndio sababu wakati
mwingine ni kupata vitu kinyume cha matukio hayo
kutafungua furaha tena maishani.
M: Kweli kabisa. Maumivu ya moyo usiseme wala usiombee....
yanamtafuna mtu polepole na kuwa kama mchwa anavyotafuna
gogo... unashangaa siku moja gogo kubwa la mti
linadondoka...na kuacha watu wakishangaa. Lakini si ndio
maisha Freddy:? kuna mabonde, milima, mito,miteremko
nakadhalika
Y: Ni kweli lakini katika maisha hatutafuti mabonde na milima
tunatakiwa kutafuta na kukwepa hayo na hatutakiwi
kuyalazimisha. Na ni vizuri kuhakikisha hatuwi hivyo kwa
watu wengine. I promise my dear sitakuwa mlima na na
mabonde kwako!
M: Hahaha Freddy, hebu acha utani... unajua una utani sana
wewe huwezi kutabiri...unajua mwanzo wa kila uhusiano kuna
ahadi nyingi sana. Umenikumbusha kitu..
Y: Nimekukumbusha nini Darling?
M: Hahahahahhah...
Y: Mbona unanicheka tena?
M: Sikucheki wewe mpenzi...najicheka mwenyewe lakini hebu
tuyaache hayo...
nataka tuongee yetu.
Y: Haya we, niko wako wangu. Una siri nyingi wewe!
Unajipamba kwa ajili ya kesho?
M: Mhhhh.... kujipamba... hiyo muhimu. Si unajua tena
mwanamke kujipamba ni wajibu.
Y: Unanitamanisha kwa hilo wazo tu. Ulinitamanisha sana jana
na sasa nataka kuchonga mzinga kabisa.
M: Ni nini kilikutamanisha zaidi.... hebu niambie ukweli
mpenzi
Y: Kwanza una macho mazuri sana, sauti yako ndio kabisa, na
una namna ya kunifanya niwe kama kipepeo kwenye mshumaa
wa moto, naungua na kuteketea mbele zako.
M: Hahahahah wewe bwana!! Una maneno wewe! Tena
mazito.... hebu niambie ukweli wako..Who is Freddy?sidhani
huyu Freddy nimeshamfahamu... there is something that u r not
telling me, u sound kama mshairi, mtunzi n.k
Y: Unataka kujua nini hasa?
M: Hebu nipe historia fupi ya maisha yako.... kuna mystery
fulani about you.
Y: Utajua mengi ukiwa umelala pembeni yangu kesho usiku;
nitajibu maswali yako yote. Naomba nibakie hivyo hivyo
"mysterious". Hata mimi nahisi kuna siri nyuma yako na
natamani uniambie kila kitu.
M:
Hahaha...you
are
impossible!
lakini
kama
unavyosema..tutapata muda wa kufahamiana zaidi.
Y: Siyo kufahamiana tu, kujuana kabisa! In the biblical sense!
LOL
M: hahaha ati kujuana! we mchokozi kwelikweli! I won’t mind
unijue!
Y: Ndiyo kujuana kabisa, nataka nijue kila nchi ya mwili wako,
kila chembe ya ngozi yako, kila mguno, kila sauti, kila utamu
na kila kitu thats you!
M: oh my! unanimaliza kwa maneno yako mpenzi. Unanigusa
kwa nmna ya pekee. Sikumbuki ni lini liwahi kujisikia hivi
tena baada ya miaka mingi sana.
Y: natumaini utakuwa ni mwanzo tu wa safari ndefu ya furaha
ya mapenzi kati yangu na wewe. And I’m looking forward!
M: Nahitaji furaha hiyo..nahitaji kujisikia napendwa... nahitaji
nami kupenda, kumpenda mtu atakayeitikia pendo na mapenzi
yangu.....mwenye
kuthamini
penzi...
mwenye
kunielewa...mwenye kunigusa hisia zangu zilizoanza kufifia
Freddie. Unanielewa lakini?
Y: Nakuelewa kila kitu Tina, najisikia pungufu mbele zako
nataka ni kupe mapenzi yangu yote. Sijui kama nastahili.
Najiuliza katika mawazo yangu ninastahili vipi moyo wako?
Nastahili vipi hata kukugusa. Ni kama mtumwa kukaribishwa
chumbani kwa malkia, nitawezaje kuvuka kizingiti cha
mlango?
Nilipoyasoma maneno hayo nilijisikia uchungu. Yalinigusa
moyoni na kunifanya nijisikie mnyonge. Sikutaka kijana huyo
ajisikie duni mbele zangu. Maneno yake yalikuwa kama
misumari ya moto. Nilitamani angekuwa karibu nimhakikishie
kuwa upendo haujali hayo mengine yote.
M: Jamani Freddy! usinitie unyonge, kwanini unasema hivyo?
Y: Ningekuwa katika sehemu nyingine nisingeshangaa lakini
hii bahati hii kwanini naistahili mimi? Clementina unaweza
kuwa na mtu yeyote unayemtaka au anayekutaka na nina
uhakika wapo wengi ambao wangeweza kabisa kuwa na wewe,
kwanini mtu kama mimi? Hii unajua kina dada wangapi
huwawanapita pale kibandani wakiona rasta zangu tu wanaona
ni "mvuta bangi"? na hata hawanitazami tena?
M: Kwani hata ingekuwa malkia..milango si inaingilika tu?
umesahau kule Uingereza miaka ya 90? Unajua maisha yako
complicated. Kuna so many people who are so lonely
hutajua mpaka usikie hadithi zao hao wanaokupita kila siku
pale kibandani huenda wana matatizo yao mengi mno kiasi
kwamba.... hitaji la kumpenda mtu ni kitu cha mwisho
kukifikiria au hitaji la kupendwa siyo kipaumbele. Unanipata
lakini?
Y: Nakupata, unajua sijawahi kufikiria hilo. Mara nyingi
nafikiria wanaringa na wana nyodo, au ndio mbwembwe
zenyewe au ndiyo yanaitwa mapozi! Kumbe huwezi
kuwahukumu watu kwa kuwaangalia tu.
M: Usihukumu kabisa! Mimi nimeshajifunza hili somo siku
nyingi! Zamani nilikuwa na vipimo vyangu vya kupima watu
na mambo wayafanyayo siku hizi nimeacha kabisa kwa sababu
kila kitu kinachofanywa na binadamu kina maelezo tena
pengine mazito yenye kuingia akilini sana. Huwezi kuhukumu
mtu na matendo yake kwa kutumia kipimo standard kwa watu
wote.
Y: Jamani Clementina umejaa hekima kama ulivyojaa uzuri!
M: Mbona hata mimi nakuona una hekima sana..ndio maana
pale mwanzo nikakuuliza huyu Freddy ni nani ? maisha yana
mengi ndani yake...ndio maana wenzetu husema " live your life
to the fullest"
Y: Kwa kweli with you now.. I intend to. Nilikuwa nimekata
tamaa sana na maisha.
M: ni kwa sababu watu tunaishi sehemu ndogo sana ya maisha
yanavyotakiwa yawe kwa sababu mbalimbali. Unanishawishi
kuendeleza swali langu kwako.... who is this Freddy jamani?
Nilituma ujumbe huo kabla sijasoma ujumbe wake wa awali.
Nilipouona ulinigusa na kunishtua kidogo.
M: Ulitaka kukata tamaa kwanini?
Y: Kwa sababu sikuamini mtu anaweza kuingia katika maisha
yako na kupindua kabisa fikra zote ulizokuwa nazo kuhusu
mapenzi.
M: oh... tell me more, please.
M. Hata mimi tena zaidi. Nashukuru kunipa kampani.
Y: Tina, naweza kukuomba kukuuliza jambo moja very
private?
Moyo ulinidunda tena, sijui anataka kuniuliza nini.
Ulipita muda na muda ulikuwa umeanza kukaribia kwenye saa
tano hivi ili nianze msafara wa kwenda Saloon. Nilishangaa
mbona amechelewa kunijibu.
M: Freddy, umekaa kimya.... nimekukumbusha kitu kibaya?
haya tuache topic hii...
Y: Jamani, hapana mtoto alikuwa ananisumbua hapa kidogo.
Tutazungumza sana huko mbeleni Tina usiwe na shaka.
M: Mtoto? una mtoto?
Y: Ndiyo wa miaka 6 aliachwa na mama yake.Nilikuambia
jana umeshasahau?
M: Sikumbuki..si unajua jana. Jana ilikuwa siku tofauti sana.
LOL
Y: Kweli nilikuchanganya wangu. Sasa ya kesho kweli ndio
utakumbuka?LOL
M: Jamani..unaninyanyasa sasa! leo nimeshatulia..nitakumbuka
Y: Hahaha sawasawa. Basi nikuache na miye nijiandae hapa na
shughuli fulani fulani, nakusubiri kwa hamu sana kesho.
Ukipata muda usiku nipigie nina hamu ya kusikia sauti yako
kabla sijaenda kulala maana jana ulinipa ndoto tamu sana!
M: sawa mpenzi, na miye naelekea Saloon! Kuna sherehe
kubwa kesho.
Y: Oh yeah, wapi tena?
M: Si kwako!
Y: Safi kabisa, tuna mengi ya kuongea basi. Nimefurahi sana
kuchat na wewe darling
M: Uliza tu usiwe na shaka.
Y: Naomba ukija uje ukiwa umenyoa nywele zote za mwili
ubakie na hizo za kichwani tu
M: Mmmh.. yaani zote?
Y: Ndiyo zote, if you don’t mind. Si unajua mambo ya
Brazilian?
M: Ndiyo.
Nilijihisi kutetemeka. Sikuelewa alikuwa anafikiria vitu gani
au ameniuliza hivyo kwa sababu gani. Lakini aliuliza kwa
namna nzuri kiasi kwamba vyovyote alivyokuwa anafikiria
nilikuwa niko tayari.
Y: Basi hilo tu nakuomba, hutajutia.
M. Done.
Tuliagana kwa maneno mengine na mimi nikajiandaa kutoka
pale nyumbani na kuanza kuelekea Saloon ya Bantu maeneo ya
Morocco/Kawawa karibu na Pub ya PR. Moyoni nilikuwa na
wazo moja tu nalo lilikuwa Jumamosi. Nilipanga nitakaporudi
nyumbani kutoka Saloon nijifungie bafuni nijinyoe kila kitu.
Nilijicheka nilipowasha gari kwa mawazo hayo. Lakini
nilipania lolote litakalokuwa, lazima nishiriki kikamilifu katika
sherehe za Muungano.
Siku ilikuwa inaenda pole pole mno nilijiambia nikiishika
barabara ya Morogoro. Ningekuwa na uwezo ningeiruka
Ijumaa niwe Jumamosi! Nikakumbuka msemo wa wahenga.
Mvumilivu hula mbivu. Au huliwa!
***
Download